Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

Hili ndiyo kosa moja kubwa unalofanya kwenye mshahara wako unaopokea kila mwezi.

Kwa mshahara ah kipato chochote unachopokea, iwe ni malipo ya kazi zako binafsi au faida unayotengeneza kwenye biashara, kuna kosa moja kubwa umekuwa unalifanya. Kosa hilo ni KUMLIPA KILA MTU NA KUJISAHAU WEWE MWENYEWE.
Hebu fikiria unapopata fedha unaanza na nini? Kulipa madeni, kulipa bili, kununua vyakula, kununua nguo, kulipia starehe na mapumziko mbalimbali. Baada ya siku chache za kupata fedha unakuwa umeimaliza yote, huku wewe ukibaki mtupu kabisa.
Sasa rafiki, jua kwamba huwezi kuwa huru kifedha kama utaendekeza utaratibu huo wa kuwalipa wengine na kujisahau wewe mwenyewe. Kwenye kila kipato unachoingiza, mtu wa kwanza kumlipa unapaswa kuwa wewe.
Najua hapa huelewi vizuri, kwamba unajilipaje, na hayo matumizi si ndiyo kujilipa? Jibu ni hapana. Na hapa nitakuomba ufanye rejea kwenye kitabu cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA, kwenye kipengele cha DHANA YA KUJILIPA WEWE MWENYEWE KWANZA.
Kama mpaka huna kitabu hicho, piga simu au tuma ujumbe kwenda namba 0678 977 007 na utaletewa au kutumiwa kitabu ulipo.
#SomaVitabuTanzania

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.