Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

REKODI YA ELIUD KIPCHOGE IMEFUTILIWA MBALI NA SHIRIKISHO LA RAIDHA DUNIANI IAAF



Licha ya Mwanariadha Eliud Kipchoge kuvunja rekodi yake mwenyewe na kuandikisha historia kwa kuwa mwanadamu wa kwanza kukimbia masafa ya kilomita arubaini na mbili kwa kutumia muda wa saa moja dakika hamsini na tisa na sekunde arubaini duniani,shirikisho la riadha duniani IAAF linasema kuwa halitatambua rekodi hiyo.
Kwa mjibu wa jarida la Game yetu la sharika la The standard,IAAF inasema kuwa sheria saba za shirikisho hilo zilivunjwa katika riadha hizo.
Baadhi ya sheria zilizovunjwa kwa mjibu wa IAAF ni kuwa.
1.Wanariadha wasaidizi maarufu pacemakers,hawafai kubadilishana kama ilivyoonekana katika mbio hizo za leo.
2.Lazima kuwe na uchunguzi wa dawa za kusisimua misuli kabla ya shindano lolote,ili hali halikuwepo.
3.Vinywaji vinafaa kuchukuliwa katika vituo vilivyoidhinishwa bali sio mwanariadha kuletewa kama alivyoletewa Kipchoge.
4.Lazima kuwa na angalau wanariadha watatu wanaoshindana,ili hali Kipchoge hakuwa na mpinzani hata mmoja.

5.Mwanariadha hafai kudhibitiwa na gari ambalo lina kidhibiti kama ilivyoonekana katika hafala ya kipchoge hii leo.
6. Shindano hilo linafaa kufuatiliwa,kuidhinishwa na kutuzwa na afisa aliyeidhinishwa na shirikisho la IAAF.

About KELVIN WILLIAMS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.