Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

Wezi watoweka na mbuzi 33 katika kijiji cha Yatia eneobunge la Baringo kaskazini siku moja baada ya onyo kutoka kwa mshirikishi wa kanda George Natembeya

Saa chache tu baada ya mshirikishi wa masuala ya serikali kuu katika iliyokuwa mkoa wa bonde la ufa George Natembeya kuzuru kaunti ya Baringo na kutangaza vita dhidi ya wezi wa mifugo,kundi moja la wezi waliweza kuvaamia tena kijiji cha Yatia kwenye eneobunge la Baringo kaskazini usiku wa kuamkia leo,na kutoweka na mbuzi 33 kuelekea eneo la Che-si-ri-mion kwenye eneobunge jirani la Tiaty.
Christopher Cherogony ambaye ni mwaadhiriwa wa kisa hicho cha mavaamizi anasema wezi hao walifika nyumbani kwake mwendo wa saa tano za usiku,na kufungulia mbuzi wake na kwa kuhofia usalama wake,yeye na familia yake waliamua kutulia ndani ya nyumba hadi wezi walipoweza kuondoka.
Kisa hicho kimeibua wasiwasi mwingi wa kiusalama katika eneohilo,huku Richard  Chepchome ambaye ni mkereketwa wa maswala ya amani katika kaunti hiyo akitoa wito kwa serikali kuendesha operesheni ya dharura katika eneohilo,kama alivyokuwa ameahidi bwana Natemebeya.
Alipohutubu mjini Kabarnet,Natemebeya aliweza wazi kwamba serikali inaweka mikakati za kubuni kambi ya kuendesha operesheni katika maeneo zinazokumbwa na usalama,huku akionya kwamba machifu watabeba msalaba iwapo mifugo walioibwa watapitishwa katika maeneo yao.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.