Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

ELGEIYO MARAKWET:Wafanyakazi walalamikia kucheleweshwa kwa mshahara wa mwezi Julai.

Chama cha wafanyakazi humu nchini tawi la kaunti ya Elgeyo Marakwet limeitaka  serikali ya kaunti hiyo kushugulikia malipo yanayokatwa kutoka kwa mishahara yao ili kuwaondolea faini na riba kutokana na kuchelewa kulipwa kwa mikopo kwenye benki.

Pesa hizo zinazokatwa ni pamoja na zile za kulipia mikopo kwenye benki, bima ya afya  ya matibabu NHIF, hazina ya kusimamia pesa za uzeeni NSSF pamoja na lap fund.

Wakiongozwa na katibu wa chama hicho James Kangogo, wafanyakazi hao wamesikitishwa na hatua ya serikali ya kaunti hiyo ya  kuchelewesha malipo hayo ya mwezi wa Julai kwani huenda ikatatiza shughuli zao za kawaida pamoja na maendeleo ya kibinafsi.
  
Hata hivyo, wafanyakazi hao wanataka serikali ya kaunti hiyo pamoja na bunge la kaunti hiyo kusitisha malumbano kati yao haswa katika utengenezaji wa bajeti ili kuepukana na migomo inayoshuhudiwa kila mara.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.