Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

HATUTISHWI,TUTAHAKIKISHA MSITU WA MAU UMEHIFADHIWA:Asema Mratibu wa kanda ya bonde la ufa George Natembeya

Mratibu wa kanda ya bonde la ufa George Natembeya ametangaza kufungwa kwa shule kumi na tano katika msitu Mau ambazo amesema zimekuwa zikihudumu kiharamu.
Akiongea afisini mwake mjini Nakuru  Natembeya amesema hii ni mojawapo ya hatua katika awamu ya pili ya kuwaondoa waliongia msituni humo .Amesema takriban familia elfu kumi zitaathirika na zoezi hilo.
Kamishna huyu vilevile amedokeza kuwa serikali inalenga kurejesha ardhi hekari kumi na saba elfu zilizonyakuliwa kwa jumla ya hekari arobaini na sita elfu za msitu Mau.
Wakati   uohuo Natembeya amesema kuwa wameanzisha mpango wa kuweka ua wa umeme sawa na kuongeza alama zinazowekwa kudhihirisha mipaka ya ardhi maarufu beacons katika juhudi za kuhifadhi msitu huo.
Ameahidi uwepo wa maafisa wa kutosha katika shughuli hiyo nzima.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.