Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

KAKA ISAAC, NGULI WA MZIKI AJITOKEZA LICHA YA KUPITIA MAISHA YA UMASKINI



"Mungu ni mwaminifu,ukimwamini na kumtegemea kwakweli hatakuwacha"  Ndiyo matamshi  ya kwanza kutoka kwa chipukizi huyu wa nyimbo za injili aliyepata fursa hadimu  kuzungumza na jarida hili la  The Superstar.
Kaka Isaac kama anavyo julikana na wengi katika sanaa yake ya mziki ni  kijana aliyezaliwa kutoka familia ya uchochole  mjini Kitale katika  kijiji cha Matisi.
Anasema kuwa  maisha yamemfunza mengi ambayo hakuwa anajua kama angefaulu kuyashinda na kuwa hai leo na vile vile kunawiri katika usanii jinsi alivyo kwa sasa.
Mziki sio rahisi haswa msanii anapokosa usaidizi wa kifedha,mara nyingi wasanii wengi wamekosa kusikika ama kung'aa kwa kukosa fedha za kurekodi miziki yao,lakini kwa Kaka Isaac  umaskini na ufukara haukumzuia kuifuata na kutimiza ndoto yake,Anasema "Mimi nililelewa katika jamii fukara iliyotengwa na wote waliotuzunguka,watu walituona kama wasiofaa,maana hatukuwa na pesa wala heshima ,tulitumiwa kama mfano mzuri wa watu waliofeli katika maisha" aliongeza kuwa  babake mzazi  alipofariki jamii ikawatenga,maisha yakawa magumu sana, walikula kwa kukota na kuomba omba mitaani kutoka kwa wasamaria wema.

Lakini mungu si athumani,wala hamsahau mja wake, maana  hakumuawacha Isaac kupitia katika huduma yake  wa uimbaji .
Isaac ambaye sasaa amewashangaza wengi amefanya album ya kwanza  na anaaminui kuwa  na nyingi zaidi.
Nyimbo zake zinapatikana kwa sasa katika YouTube  kupitia jina Kaka Isaac

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.