Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

MWALIMU AACHILIWA KWA DHAMANA YA SHILINGI ELFU 300 BARINGO KWA TUHUMA ZA KUMNAJISI MWANAFUNZI WA DARASA LA SABA



Mwalimu wa shule ya msingi ya Chebore iliyoko katika eneobunge la Baringo kaskazini ameachiliwa kwa dhamana ya shilingi elfu 300 hii leo na mahakama ya Kabarnet,baada ya kushtakiwa kwa kosa la kumnajisi  mwanafunzi wake wa darasa la saba.
Mshukiwa kwa jina Allan Cheburet kutoka wadi ya Barwessa alifikishwa mbele ya hakimu mkaazi wa Kabarnet Vienna Ambogo, na kushtakiwa kwamba mnamo tarehe 31 mwezi uliopita wa saba mwaka huu wa 2019 katika kituo cha kbiashara cha Barwessa,yeye aliweza kumhadaa mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 13,na kumdhulumu kimapenzi mwendo wa saa saba za mchana.
Mshukiwa aliweza kukana shtaka hilo na kuachiliwa kwa dhamana hiyo ambapo,atatarajiwa kufika mahakamani tarehe 14 mwezi huu wa Agosti ambapo kesi hiyo itaweza kusikizwa.
Kesi hiyo imewasilishwa siku moja tu baada ya mshtakiwa mwingine kwa jina David Kipkemoi kuwasilishwa kwenye mahakama jana Alhamisi,na kushtakiwa kwa kosa la kumnajisi mtoto msichana mwenye umri wa mwaka mmoja,katika kijiji cha Kaptimbor kilichoko viungani mwa mji wa Kabarnet.
Mshukiwa huyo aliweza kuzuiliwa na kutarajiwa mahakamani tarehe 13 ambapo kesi yake itasikizwa rasmi.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.