Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

MAU:Shughuli zote sasa zimesitishwa katika msitu wa Mau

Hamna shughuli  zozote zitakazoendelezwa katika msitu wa Mau kulingana na kamisha kanda ya bonde la ufa George Natembeya .
Akiongea na wanahabari Natembeya amesema kuwa  mjadala kuhusiana na  kuondolewa kwa wanaoishi katika msitu huo umezidi kuzua  hisia mseto miongoni mwa wananchi jambo ambalo lazima lishughulikiwe kikamilifu.
Kamishna huyo anasema Serikali kupitia kamati ya watu kumi inayowahusisha  wadau inatarajiwa kuanza shughuli hiyo ya siku sitini katika  eneo la  kusini mwa Mau.
Natembeya amesema haya baada ya kikao na wadau hao akidokeza kuwa serikali vilevile inapanga kuweka ua wa umeme kama njia moja ya kuzuilia shughuli za kulima na hata kuingiza mifugo kwenye msitu huo.  
Vile vile amewarai wanasissa kushirikiana na serikali kufanikisha mpango huo akikana madai  kuwa serikali ilitoa  hati miliki katika ardhi ya msitu ambayo ni vyanzo  vya maji nchini.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.