Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

NAIVASHA:Seneta wa Nakuru Susan Kihika alaani vikali kunyanyaswa kwa wachuuzi Naivasha

Mbunge wa Gilgil Martha Wangari na Seneta wa kaunti ya Nakuru Susan Kihika sasa wamesema watapeleka mswada bungeni ili kupunguza faini zinazotozwa kwa wale wanaofanya makosa madogo.
Wakizungumza wakati wa hafla ya kuchangisha pesa kwa wachuuzi waliotiwa nguvuni wiki jana iliyopita katika eneo la kupima uzani wa magari la Gilgil, wawili hao wamesema kuwa sheria ya sasa ilikuwa finyu kwa wale wenye makosa yasiyofaa kifungo cha jela.
Kulingana na Wangari hatua ya kushikwa na kufikishwa mahakamani kwa wachuuzi hao baada ya kuondolewa kwa lazima eneo hilo na shirika la kusimamia barabara za kitaifa haikufaa hata kidogo.
Mbunge huyo amesema wachuuzi hao walikuwa wakitafuta lishe kwa familia zao kwa kuuza bidhaa kama vile maji na walifaa kusaidiwa badala ya kuwaondoa.
Naye Kihika amekemea hatua hiyo na kusema wachuuzi hao walitozwa faini ambazo hawawezi kuzikimu kwani wengi ni maskini wanaoishi katika vitongoji duni vya Gilgil.
Wengine waliozungumza ni pamoja na mwakilishi wa wadi ya Giglil Jane Ngugi na viongozi wengine wa mji huo.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.