Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

Wanafunzi wapatao 500 wa chuo kikuu cha Moi wameandamana kulalamikia usimamizi duni wa chuo hicho

 
 
Wanafunzi wapatao 500 wa chuo kikuu cha Moi wameandamana baada ya majina yao kukosa kwenye orodha ya watakaofuzu wakiilaumu usimamizi wa chuo hicho kwa kutoshughulikia swala hilo.

Wanafunzi hao waliopiga kambi kwenye chuo hicho, wamesema kuwa wamekuwa wakipitia changamoto  kwa miaka mingi bila usimamizi wa chuo hicho kutafuta suluhu.

Wamedai kuwa, baadhi yao wangekuwa wamefuzu miaka miwili ama tatu zilizopita lakini chuo hicho kimekuwa kikihairisha wakati wao wakuhitimu huku wakiongezea kuwa, wakati mmoja wanaosimamia usalama chuoni humo waliwafurusha nje ya chuo hicho.

Sasa wanataka majina yao yajumuishwe na ya wanafunzi wengine watakaofuzu mwezi huu la sivyo, watafika mahakamani kusimamisha sherehe ya kufuzu inayotarajiwa kufanyika mnamo tarehe 22/08/2019.

Juhudi za kuwafikia wasimamizi wa chuo hicho cha Moi ziligonga mwamba.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.