Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

Miili 25 iliyowachwa kwa takriban miezi 6 bila kuchukuliwa katika hifadhi ya maiti ya hospitali kuu ya kaunti ndogo ya Naivasha kuzikwa kwa kaburi la umma



Idara ya afya na usafi wa umma imesema kuwa itaizika takriban miili 25 katika kaburi la umma mjini Naivasha baada ya kupata idhini la mahakama.
Miili hiyo imekuwa kwenye hifadhi ya maiti ya hospitali kuu ya kaunti ndogo ya Naivasha kwa zaidi ya miezi sita bila ya kuchukuliwa.
Kulingana na mkuu msimamizi wa hospitali hiyo Dkt Angeline Ithondeka, hatua hiyo itapelekea wao kupunguza fedha wanazotumia kuifadhi miili hiyo hospitalini.
Ithondeka amesema miili hiyo na ambayo itazikwa katika makaburi ya umma huko Longonot ililetwa kutoka sehemu tofauti huku ile mingi ikiwa ya wahanga wa ajali zinazotokea kwenye barabara kuu ya Nakuru kuelekea Nairobi, Mai Mahiu kuelekea Naivasha na Mai Mahiu kielekea Narok.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.