Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

Wawakilishi wadi kutoka kaunti ya Nakuru wadai kushurutishwa na serikali kuu kuangusha mswada wa Punguza mzigo

Wawakilishi wa wadi katika kaunti ya Nakuru wamesema baadhi ya maafisa wakuu wa serikali ya kitaifa wameanza kuwapa vitisho ili kuweza kuangusha mswada wa Ekuru Aukot wa Punguza mzigo unaolenga kubadilisha katiba ili kuondoa nyadhifa Fulani.
Haya yamejiri huku wawakilishi hao wakiitwa kwa mkutano katika hoteli moja mjini Naivasha na kuarifiwa madhara ya mswada huo huku kikao na wanahabari walichokuwa wamepanga kikikosa kufanyika kwa dakika ya mwisho.
Wengi waliozungumza na kituo hiki japo hawakutaka kutajwa majina yao wamesema wanashurutishwa kuangusha mswada huo huku wakiletewa watu waliojitaja kama wataalamu wa maswala ya katiba ili kuambiwa madhara hayo.
Hata hivyo aliyekuwa kiongozi wa wengi katika bunge la kaunti hiyo Stanley Karanja amesema kuwa mkutano huo umejadili maswala mengi yakiwemo yale ya mikopo ya magari yao na malipo ya uzeeni kwa wafanyikazi wa serikali hiyo kati ya maswala mengine.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.