Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

Ukosefu wa maji umeghubikia wakazi wa maeneo ya Eburru, Morgan, Kongasi, Nagum na Gema kaunti ndogo ya Gilgil baada ya bwawa la Thome lililokuwa likiwapa maji kupasua kingo zake na kumwaga maji


Hali ya upungufu wa maji umeghubikia wakazi wa maeneo ya Eburru, Morgan, Kongasi, Nagum na Gema kaunti ndogo ya Gilgil baada ya bwawa la Thome lililokuwa likiwapa maji kupasua kingo zake na kumwaga maji.
Viongozi eneo hilo wakiongozwa na kiongozi wa wanawake Lydia Nyota wameelekezea kidole cha lawama kwa mwanakandarasi aliyepewa kazi ya kukarabati bwawa hilo kwa utepetevu kazini.
Nyota amesema japokuwa eneo hilo halikuwa na mvua wakati wa mkasa huo haijabainika kilichofanyika na mwanakandarasi huyo na kupelekea tatizo hilo kufanyika.
Hata hivyo naibu wa kamishna wa kaunti ndogo ya Giglil Mutheki Ndambuki amedhibitisha tukio hilo na kusema wahandisi kutoka serikali ya kaunti ya Nakuru wametumwa kuangalia hali ya sasa ya bwawa hilo japokuwa hakuna aliyejeruhiwa.

About KELVIN WILLIAMS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.