Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

Gavana Lee Kinyanjui wa Nakuru kubuni jopo la kunyakua ardhi zilizotwaliwa na maafisa wa serikali kinyume cha sheria

Serikali ya kaunti ya Nakuru imeanza mpango wa kuchukua ardhi zilizokuwa zimenyakuliwa na watu waliokuwa na usemi mkubwa serikali za awali.

Akizungumza baada ya kuzuru mji wa Naivasha kukagua miradi ya maendeleona kuanzisha mradi wa ujenzi wa soko la kisasa la mji huo, Gavana Lee Kinyanjui amesema amebuni kamati itakayo chunguza ardhi hizo na kutoa ripoti kikamilifu kabla ya kutekeleza agizo hilo.

Kulingana naye, imekuwa vigumu kutekeleza miradi ya serikali kwani maeneo wanayokisia kufanya hivyo yamenyakuliwa na watu wanaodai kuwa na hati miliki ya ardhi ili wafidiwe tukio ambalo amesema ni kinyume cha sheria.

Vile vile Kinyanjui ametoa ilani kwa wanakandarasi wanaochelewesha miradi waliyopewa kufanya kuwa wataachishwa kazi hiyo iwapo watapatikana kuwa wana uzembefu kumaliza miradi waliyopewa.


About KELVIN WILLIAMS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.