Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

Gavana wa Baringo na mwenzake wa Pokot Magharibi washirikiana kurejesha amani katika maeneo yao

Gavana wa Baringo Stanley Kiptis na mwenzake wa Pokot Magharibi John Lonyangapuo wameanzisha juhudi za kurejesha amani katika bonde la Kerio,na kuhimiza jamii zote za wafugaji kuungana na kuleta maendeleo.
Wakizungumza jana katika eneo la Kolowa kwenye eneobunge la Tiaty,Gavana Kiptis anasema viongozi wa maeneo zinazokumbwa na tatizo la utovu wa usalama wana jukumu la kuzungumza kwa sauti moja,na kupinga vitendo vinavyohujumu maendeleo.
Kiptis anahimiza ujumbe wa amani kusambazwa hadi mashuleni,huku akihimiza serikali kuu na wadau wengine wa maendeleo kubadilisha fikira kuhusu ukanda mwa kaskazini mwa bonde la ufa kama eneo hatari.
Aliyekuwa mbunge wa Tiaty Asman Kamama,seneta Kipchumba Murkomen,mbunge wa Kapseret Oscar Sudi miongoni mwa wengine waliweza kuhudhuria kikao hicho cha amani.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.