Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

Msirikishi wa kanda ya bonde la ufa George Natembeya ametangaza vita vikali dhidi ya wezi wa mifugo

Mshirikishi wa masuala ya serikali kuu katika eneo la  bonde la ufa Goerge Natembeya ametangaza vita vikali dhidi ya wezi wa mifugo ambao wanazidi kutatiza usalama katika eneo la Baringo kwa kuiba mifugo.
Akihutubu mjini Kabarnet ambapo aliweza kukutana na wakuu wa usalama kwenye kaunti hiyo,Natembeya ameapa hadharani kwamba serikali iko tayari kuwakabili wezi wa mifugo katika eneo la Baringo,Samburu,Laikipia na pia Turkana,akaelekeza wakuu wa kaunti hizo kubuni mwongozo wa kuendesha operesheni hiyo haraka iwezekanavyo.
Wakati huo huo ,Natembeya ametoa  makataa ya hadi jumamosi kwa machifu kurejesha ngombe 55 waliobiwa hivi karibuni kutoka eneobunge la Baringo kaskazini,huku akionya kwamba machifu watapoteza mifugo wao iwapo watakosa kushirikiana na serikali kukabili tatizo hilo la wizi.
Natembeya ametangaza msimamo huu wakati ambapo waadhiriwa wa utovu wa usalama katika maeneo ya Marigat na Baringo kaskazini wanaonekana kupoteza matumaini ya kuishi kwa amani,kufuatia msururu wa mashambulizi kutoka kwa wezi wa mifugo ambao wameponekana kupata nguvu mpya,baada ya serikali kutwaa bunduki zilizokua zikitumika kutoa ulinzi kwa wananchi na mali yao,kupitia kwa askari wa akiba NPR.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.