Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

KIAMBU-Gavana Ferdinand Waititu huenda akakamatwa tena na kuzuiliwa



Wanaharakati wakiongozwa na Suba Churchil sasa wanataka idara ya jinai kumtia mbaroni na kumzuilia tena gavana wa kiambu Ferdinand Waititu kwa kukiuka maagizo ya mahakama baada ya kuwachiliwa kwa dhamana ya shilingi milioni 15 juma lilipita.
Wamemkashifu gavana huyo kwa ziara yake wikendi  kwenye maeneo ambayo miradi anayohusishwa nayo katika kesi ya ufisadi na utumizi mbaya wa mamlaka  inatekelezwa kando na kuhutubia halaiki ya watu.
Wanasema kuwa hatua hiyo ni kuhitalifiana na ushahidi dhidi ya kesi inayomwandama.
Hata hivyo gavana huyo amekinzana na wanaharakati hao huku akitaja kuwa bado yuko na  mamlaka ya utendakazi kama gavana licha ya kuwekewa ilani ya kutofika afisini mwake.
Anasema kuwa mamlaka yake hayako afisini wala kwa gari lake la serikali na hivyo atazidi kuwahudumia wananchi licha ya kukosa afisi.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.