Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

KISUMU- Serikali ya kaunti ya Kisumu yanunua Prado kuu kwa shilingi milioni 19



Gavana wa Kisumu Prof.Peter Anyang’ Nyong’o  amelaumiwa  na wakaazi wa kaunti  hiyo kufuatia utumizi mbaya wa pesa za umma.
Hii ni baada ya kubainika kuwa kaunti hiyo ilinunua gari kuu aina ya Toyota Prado kwa kima cha shilingi milioni 19.
Kwa mjibu wa taarifa za jarida la Citizen weekly wawakilishi katika  kaunti hiyo vile vile wanahusishwa na kandarasi zinazotolewa huku ikibainika kuwa wanamiliki kampuni zinazotekeleza baadhi ya miradi kwenye kaunti huyo.
Wa hivi karibuni kukashifiwa ni mwakilishi wa wadi ya Railways David Arao  amabye anadaiwa kujenga choo katika eneo la bandari ya  Lwang’ni  kwa kima cha shilingi milioni 5.
Choo hicho hata hivyo kimebomolewa kufuatia ukarabati wa bandari hiyo.
Vile vile kuna baadhi ya viongozi wanaokisiwa kupanga mikakati ya kuvuna fedha za umma katika mradi wa kuboresha jiji hilo la Kisumu ,mradi unaofadhiliwa na banki ya dunia.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.