Afisa
mmoja wa trafiki anachunguzwa baada ya kuonekana kwenye kanda ya video akiomba
rushwa ya shilingi 1500/- kutoka kwa dereva wa taxi mtaani Eastleigh jijini
Nairobi.
Katika
kanda ya video iliyosambazwa mtandaoni dereva huyo ambaye hajatambulishwa
anasikika akimrai afisa huyo kumuonea huruma kwa kukosa fedha hizo huku akisema
hana,na itabidi aombe ndiposa apate hela
hizo.
Afisa
huyo aidha anasikikika akisema “Si
ulikua unasema uko na elfu moja. Kwa hivo haukua nayo ni kuomba ulikua unaomba
yote?
Hata hivyoo dereva huyo alilazimika
kumpa afisa huyo fedha hizo kwa mjibu wa video hiyo.
Mamlaka ya Huduma za polisi NPS
imethibitisha kupokea kesi hiyo na kuahidi kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya
afisa huyo.
Tukio hilo linatokea saa chache tu
baada ya maafisa wa jinai kumkamata afisa mwengine wa polisi mwenye hadhi ya constable
kwa jina Samuel Mutachi kutoka kituo cha polisi cha central jijini Nairobi kwa
tuhuma za kuomba hongo ya shilingi elfu 200.
Mutachi aidha alipewa shilingi elfu
35 pekee kutoka kwa wakili mmoja huku akijifanya afisa wa jinai anayechunguza
kesi ya kughushi stkabadhi.
Idara ya jinai sasa imewataka
wananchi kuwa makini na matapeli wanaojifanya maafisa wa serikali.
About VANTAGE MUSIC RECORDS
Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.