Wizara
ya kilimo imeanzisha mpango wa kupanua ardhi zinazolimwa pareto nchini kutoka
ekari elfu sita hadi ekari elfu kumi na nane katika muda wa mwaka mmoja ujao.
Akizungumza
wakati wa siku ya wakulima eneo la Eburru kaunti ndogo ya Gilgil, waziri
wa kilimo Mwangi Kiunjuri amesema kuwa kupanuliwa huko kutawezesha kenya
kuzalisha tani elfu kumi na nane za pareto na kuweza kushindana na mataifa
mengine kama vile Uchina.
Kinjuri
amesema serikali ilikuwa imejitolea kuhakikisha kuwa sekta hiyo na ambayo
ilikuwa ikileta mabilioni ya pesa kwa wakenya imefufuliwa na kuongeza kuwa
serikali ya kitaifa itatoa shilingi milioni 45 kwa kaunti ya Nakuru ili kuweza
kupanda mbegu za mmea huo zitakazopewa wakulima.
Naye
gavana wa kaunti hiyo Lee Kinyanjui amesema kuwa wametenga shilingi milioni
45 za kununua mbegu hizo na kuongeza serikali yake tayari imetoa shilingi
milioni sabini za kuboresha fani mbali mbali za kilimo katika kaunti hiyo.
About VANTAGE MUSIC RECORDS
Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.