Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

Serikali ya Nakuru yalaumiwa kwa huduma duni eneo bunge la Gilgil.



Wakulima kutoka vijiji vinne kaunti ndogo ya Gilgil wametishia kutolipa ushuru na ada zingine kwa kaunti ya Nakuru kutokana na huduma hafifu zinazotolewa.
Wakizungumza baada ya kufanya maandamano na kufunga barabara kuu ya Gilgil kuelekea Eburru, wakulima hao kutoka vijiji vya Kamunyore, Gema Catholic, Kwa Gema na Nagum wamesema eneo hilo limesahaulika kwa maendeleo kwa miaka mingi.
Kulingana na kiongozi wao Mary Waithera, barabara za maeneo hayo hazijatengenezwa kwa muda wa miaka mitano licha ya kuwa vijiji hivyo vimo kilomita kumi kutoka mji wa Gilgil.
Waithera ameongeza kuwa licha ya wao kuahidiwa kuwa barabara hizo zitakarabatiwa hakuna kilichofanyika.
Naye Mary Nungari amesema eneo hilo halina maji huku mtungi wa lita ishirini ukiwagharimu shilingi hamsini tukio linalowafanya wao kuoga mara moja kwa wiki.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.