Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

NAIVASHA-Serikali yatakiwa kuthibiti idadi ya Vituo vya kuwalea watoto (Daycares) mjini Naivasha

Viongozi mjini Naivasha sasa wamesema kuwa ongezeko la vituo vya kuwatunza watoto kwa muda maarufu kama Day care centers na ambavyo havijaidhinishwa kisheria vimechangia pakubwa kuongezeka kwa magonjwa kwa watoto eneo hilo.
Kulingana na aliyekuwa mwakilishi wa wadi ya Lake View mjini Naivasha Simon Wanango, vituo hivyo havina na leseni huku watoto wengi wanaopelekwa wakiadhiriwa na magonjwa tofauti.
Wanango amesema kuna haja ya serikali kuchunguza vituo hivyo na kuongeza ni hivi majuzi ambapo mtoto mmoja aliaga dunia baada ya kunyongwa na chakula katika kituo kimoja eneo la Karagita.
Naye katibu wa muungano wa wafanyikazi wa maua mjini Naivasha Ferdinand Juma amesema wafanyikazi wengi wa kike wana waacha watoto wao vituoni na kuelekea kazini licha ya kutambua maeneo wanakowaacha hayajaidhinishwa.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.