Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

TUKO NA UWEZO WA KUTIBU SARATANI :MADAKTARI WA MITI SHAMBA KOIBATEK HATIMAYE WATANGAZA

By Jeremiah chamakany


Wauguzi wa madawa ya kiasili katika eneobunge la Eldama Ravine sasa wanataka serikali kutambua sekta hiyo kikamilifu,na kuishirikisha katika utafiti wa madawa na tiba za magonjwa mbali mbali kama vile saratani.
Wilson Kiragu ambaye ni mkaazi wa tarafa ya Torongo katika eneobunge la Eldama Ravine amezungumza kwa niaba ya madaktari wa miti shamba wa eneohilo,na anasema ugonjwa wa Saratani ambao umeibuka kuwa janga la kitaifa ,unaweza kutibiwa kupitia kwa madawa ya kiasili.
Kiragu anataka serikali kuwekeza katika utafiti wa madawa hayo,kwa kushirikisha watafiti kutoka kwa vyuo vikuu vilivyoidhinishwa,ili kulinda haki za umiliki kwa uvumbuzi wa dawa ya kutibu ugonjwa huo.
Katika kikao cha wanasayamsi wa kituo cha utafiti kuhusu madawa KEMRI ,na kilichofanyika mwaka wa 2017 jijini Nairobi,wanasayansi kwenye kikao hicho waliweza kutambua aina 20 ya mimea au miti za kiasili nchini Kenya,na ambazo zina uwezo wa kutibu ugonjwa wa Saratani.
Katika kikao hicho cha siku tatu,Sabina Wangui Wachira wa kituo cha utafiti kuhusu tiba za kiasili kwenye kituo hicho cha Kemri alidokeza kwamba,madawa ya kutibu saratani hutengenezwa  kutokana na miti au mimea,kwa asilimia 60 .

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.