Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

Takriban wahudumu mia mbili wa sekta ya utalii barani Afrika wanatarajiwa kukongamana mjini Naivasha

Takriban wahudumu mia mbili wa sekta ya utalii barani Afrika wanatarajiwa kukongamana mjini Naivasha ili kujadili maswala ibuka ya sekta hiyo na ambayo inakabiliwa na changa moto si haba.
Mkutano huo utalenga kuangalia madhara yatakayolewa na kuanguka kwa kampuni ya kimataifa ya Thomas Cook ambayo huwaleta watalii kutoka bara Uropa hadi Afrika na pia kuangalia mbini mbadala ya kuwafikia watalii katika bara zingine.
Akizungumza na kituo hiki kabla ya kuanza kwa mkutano huo, mkurugenzi mkuu wa shirika la wahudumu wa sekta ya utalii KATA Nicanor Sabula amesema kuwa kongamano hilo litajadili kwa mapana sekta hiyo na kuona jinsi ya kuipanua kwa kutumia teknolojia za kisasa.
Mnamo Jumatatu wiki hii, kampuni ya Thomas Cook ilitangaza kumaliza biashara hiyo na kuwaadhiri maelfu ya watalii kutoka Uropa waliokuwa tayari wamelipa nauli za ndege kusafiri sehemu tofauti ulimwenguni.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.