Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

UFUNGUZI WA VIWANDA KAUNTI YA NAKURU KUTAZIDISHA NAFASI ZA AJIRA KWA VIJANA-GAVANA LEE KINYANJUI


Viongozi wa kauti ya Nakuru wamekaribisha hatua ya baraza la mawaziri ya kutenga shulingi bilioni sita nukta tano za kuendeleza mradi wa eneo lililotengewa ujenzi wa viwanda mjini Naivasha.
Wakiongozwa na gavana Lee Kinyanjui, viongozi hao wamesema hatua hiyo itapelekea vijana wengi kupata nafasi za kazi na kusema kwa sasa mradi wa reli ya kisasa ya SGR inakaribia kukamilika tukio ambalo litabadilisha maisha ya wengi.
Kinyanjui amesema kwa sasa serikali yake ilikuwa ikifanya mazungumzo na wawekezaji wa humu nchini na wale wa nchi za nje kwa madhumuni ya kuanzisha viwanda eneo hilo.
Naye mwakilishi wa wadi ya lake View mjini humo Karanja Mburu amesema wengi watanufaika na miradi hiyo eneo la Mai mahiu na kuongeza kuwa wakazi walikuwa wakiunga mkono miradi ya serikali kuu eneo hilo.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.