Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

Familia zinazoishi eneo la Kedong mjini Naivasha zimeanza kuondoka eneo hilo ili kutwaa nafasi kwa ujenzi wa miradi ya mvuke.

Familia zinazoishi eneo la Kedong mjini Naivasha zimeanza kuondoka eneo hilo ili kutwaa nafasi kwa ujenzi wa miradi ya mvuke.
Hii ni kufuatia agizo la wao kuondoka eneo hilo na kamati ya usalama ya kaunti ndogo ya Naivasha baada ya kampuni ya kuendeleza mvuke ya Akira kununua ardhi hiyo yenye ekari elfu moja ili iweze kufanya mradi huo utakaogharimu shilingi bilioni tisa.
Akidhibitisha taarifa hiyo naibu kamishna wa kaunti ndogo ya Naivasha Mbogo Mathioya amesema nyingi ya familia hizo zimeondoka, na walio salia wanatarajiwa  kuondoka katika kipindi cha siku mbili zijazo.
Akizungumza na wanahabari mjini Naivasha leo hii, Mathioya vile vile amesema familia 23 zilizokuwa zikiishi kwenye ardhi hiyo zilipewa ekari tano kila moja lakini kumekuwa na ongezeko la watu na ambao kwa sasa wanaondolewa.

About KELVIN WILLIAMS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.