Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

Mwanamme mmoja amechiliwa kwa bondi ya shilingi elfu 100,000 baada ya kupachika picha za msichana aliyekuwa mpenzi wake kwenye mtandao.

Mwanamme aliyeweka picha na video za utupu wa msichana aliyekuwa mpenziwe kwenye mitandao ya kijamii, amefikishwa  mahakamani kwa kuendeleza dhulma mitandaoni. 
Akiwa mbele ya hakimu mkuu mkaazi Martin Rabera mshukiwa Omar Seif amekanusha mashtaka na kuachiliwa kwa bondi ya 100,000.
Hii ni baada ya Seif kufahamisha mahakama kwamba ana uchungu unaomlazimisha kufanyiwa upasuaji katika hospitali ya Mpeketoni kaunti ya Lamu. 
Kundi la kutetea haki za kibinadamu la Sisters for Justice kupitia mkurugenzi wake mkuu Naila Abdhalla, lilisema mahakamani kwamba visa vya dhulma mitandaoni vinaongezeka sana kiasi cha waadhiriwa kuamua kujitoa uhai.
Abdalla anasema licha ya ongezeko hilo haswa miongoni mwa wanafunzi wa vyuo vikuu, watu wengi wanaogopa kuripoti wamedhulumiwa mitandaoni kwa kuogopa familia isijue.

About KELVIN WILLIAMS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.