Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

Mwanamme ajitoa uhai baada ya mke wake kutiwa mimba na rafiki yake wa Karibu-Naivasha

Mbiwi la simanzi limetanda katika kijiji cha Karagita mjini Naivasha baada ya mwanamume mmoja kujitoa uhai kwa kutambuwa mkewe alipachikwa mimba na rafiki wake wa karibu.
Wengi wa wakazi wa kitongoji duni hicho walipatwa na butwaa baada ya kutazama kilichokuwa kikiendelea huku wakisema kuwa mwendazake na ambaye alikuwa mfanyikazi wa kampuni moja ya maua alikuwa mtulivu na mfupi wa maneno.
Kulingana na jirani yake tuliyemtambua tu kwa jina Ouma, mwendazake alikuwa na marafiki wake wakati alipashwa habari kuhusu mimba ya mkewe na alipofika nyumbani akamuuliza mkewe na ambaye alidhibitisha taarifa kuwa mimba hiyo haikuwa yake.
OCPD wa Naivasha Samuel Waweru amedhibitisha tukio hilo na kusema mwili huo umechukuliwa na kupelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali kuu ya kaunti ndogo ya Naivasha.

About KELVIN WILLIAMS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.