Powered by Blogger.

Header Ads


Tag:

Shule ya msingi ya Bridge Interntional Eldama Ravine imefungwa rasmi na serikali.


Shule ya msingi ya Bridge Interntional Eldama Ravine imefungwa rasmi na serikali baada ya kuibuka kwamba kando na kuendesha masomo kwa mazingira ambayo si salama kwa watoto,shule hiyo pia  imekiuka masharti ya wizara ya elimu  kuendeshea  masomo humu nchini.

Akito taarifa kwa vyombo vya habari afisini mwake punde tu baada ya kuzuru shule hiyo na kuagiza kufungwa kwake,mkuu mpya wa elimu kwenye kaunti ndogo ya Koibatek Simon Peter Kemei anasema wanafunzi wapatao 103 wa shule hiyo sasa watajiunga na shule ya msingi ya St Patrick Shimoni bila masharti yoyote,huku watahiniwa wa KCPE kwenye shule hiyo wakitrajiwa kukalia mtihani wao katika shule ya msingi ya Githioro.


Kemei anasema shule hiyo ilijengwa pasipo kuzingatia usalama wa watoto,huku sita kati ya walimu wa shule hiyo wakihudumu licha yao kutosjiliw na tume ya wlimu nchini TSC.
Chini ya ufadhili kutoka kwenye wakfu wa Bill Gates na pia 
mhasisi wa mtandao maarufu wa FACEBOOK Mark Zuckerberg,shule za Bridge International zilianzishwa nchini Kenya mwaka wa 2007 kwa lengo la kuhakikisha kwamba kupitia kwa muungano wao na shule za serikali,watoto wote wanaweza kupata elimu  ya kisasa,na kwa gharama ya chini kote mashinani.
Shule hizo zenye makao yake makuu jijini Nairobi pia zinahudumu nchini Uganda ,Nigeria, India,na Liberia.

About VANTAGE MUSIC RECORDS

Hi, My Name is Hafeez. I am a webdesigner, blogspot developer and UI designer. I am a certified Themeforest top contributor and popular at JavaScript engineers. We have a team of professinal programmers, developers work together and make unique blogger templates.